Screeni ya Hamisho jipya la fedha toka Akaunti inapata malipo na stakabadhi zilizopo kutoka kwenye vitufe vya Malipo na Stakabadhi na kuziweka katika hamisho za ndani ya akaunti. Hii ni muhimu hasa unapokuwa unafanya uagizaji wa muhamala wa benki, ambao kiotomatiki huunda rekodi zinazopangwa kama malipo au stakabadhi.
Ikiwa malipo au risiti iliyorekodiwa inawakilisha uhamisho kati ya akaunti,endelea kama ifuatavyo:
Wakati wa kulinganisha malipo na miamala ya risiti (ikiwa na kiasi sawa) kuwepo, Manager itapendekeza kubadilisha hizo kuwa uhamisho kati ya akaunti.
Unapofikia kichupo cha Hamisha fedha toka Akaunti mbalimbali, Manager itaonyesha bendera ya arifa ya njano juu ya skrini ikionyesha kuwa kuna hamisho jipya la fedha toka akaunti zinazoweza kuundwa. Kubofya tangazo hili la njano kunasababisha kufika kwenye skrini ya Hamisho jipya la fedha toka Akaunti ambapo jozi za malipo na risiti zinaweza kukaguliwa na kubadilishwa kuwa hamisho za fedha kati ya akaunti.